|
Description:
|
|
Wito umetolewa kwa kila mkenya hasa viongozi kuhakikisha amani, utulivu na usalama unakuzwa kikamilifu wakati wa msimu wa uchaguzi mkuu ujao. Wito huo umekaririwa na viongozi wakuu mbalimbali wanaokongamana mjini mombasa wakiongozwa na Rais Kibaki na Waziri Mkuu Raila Odinga. Wabunge wanaohudhuria mkutano huo, wamehimizwa kukomesha siasa za uchochezi, kikabila au kimaeneo, na badala yake wakuze siasa za ujumla wa taifa. Makongamano mengine kama hayo ya amani yanatarajiwa kufanywa katika kaunti zote. |