Rais wa Kenya William Ruto, yupo kwenye shinikizo kubwa za kuwataja hadharani wabunge na Maseneta, aliodai wanapokea rushwa kutoka kwa Mawaziri na Magavana, asasi za kiraia zinasema hiyo ndio njia pekee ya kuwaaminisha wananchi kuwa, kiongozi huyo ana nia ya kupambana na ufisadi nchini humo.